MWANAMKE AMUUNGUZA MUMEWE KWA MAJI YA MOTO



 Samuel Mungai
Mwanamke mmoja anasakwa na polisi Kabete baada ya kudaiwa kumchoma mumewe kwa maji ya sima na kisha kumficha nyumbani siku tano katika kijiji cha Muthure, eneo bunge la Kabete.  Mwanamume huyo sasa anauguza majeraha hospitali

Mwanaume huyo aliokolewa na majirani baada ya siku tano za kufichwa na mkewe aliyemchoma kwa maji moto kwenye kichwa na kifua katika kijiji hicho,
Majirani walishangaa walipomkosa Bw Samuel Mungai, mwanamume waliyemjua kama mcheshi na aliyependa kileo chake na ndipo wakaanza kumsaka.  

Chifu wa eneo hilo Peter Njoroge alisema kuwa wanakijiji walimpata Bw Mungai huku amefungiwa katika nyumba yake na majeraha mabaya, ambayo yalikuwa yameanza kunuka, yaliyosababishwa na maji moto.
“Lilikuwa jambo la kusikitisha kupata mwanaume huyu amechomeka vibaya sana kwenye kifua na kichwa,” alisema Chifu Njoroge.
Mwanaume huyo, Bw Mungai alihadithia yaliyomsibu kabla ya wenyeji kumpeleka katika kituo cha polisi cha Kikuyu kuandikisha ripoti ya uhalifu wa kinyama aliofanyiwa na mkewe, Joyce Wakanyi. Ripoti kwa polisi ilisema kuwa, siku ya Jumamosi, mwanaume huyo alifika nyumbani kama kawaida na kupata mkewe nyumbani. Shida ilizuka nyumbani wakati Bi Wakanyi aliuliza mwanaume huyo, ambaye anafanya kazi ya useremala kama alikuwa na kiwango fulani cha pesa ambacho alihitaji. La kushangaza ni kuwa, bwana huyu alisema kuwa hakuwa na pesa hizo, Sh1,000, ambazo mkewe alihitaji, lakini alikuwa amelewa, hali ambayo majirani walithibitisha kuwa  anapenda kunywa pombe sana.
Kwa hasira, inadaiwa baadaye mkewe alichukua maji yaliyokuwa kwenye jiko ya kupikia sima na kumwagia mumewe aliyekuwa amelala.



Wawili hawa, Bw Mungai na Bi Wakanyi wameishi kama mume na mke kwa zaidi ya miaka 18 na wako na watoto wanne.
Wanakijiji walifanya mchango wa harambee na kupeleka mwanaume huyo hadi Hospitali ya Wilaya ya Tigoni ambako anaendelea kupata matibabu.
Chifu Njoroge alisema kuwa si mara ya kwanza mwanamke huyo kumdhuru mumewe.
“Kuna wakati alimchapa na kumvunja mguu na mara nyingine kumuumiza mbavu,” alisema.
“Nina  hofu kuwa suluhu isipopatikana kukomesha ugomvi katika boma hili, watapata kuuana,” aliongeza Chifu Njoroge.
Mwanamke huyo, Bi Wakanyi, anasakwa na polisi baada ya kutoroka na kuacha watoto wake nyumbani huko Muthure.
 Duh! hatari kweli kweli
Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger