WANAMGAMBO WALIPUA DARAJA LINGINE LA PILI NIGERIA


Raia nchini Nigeria wakiandamana wakitaka wasichana waliotekwanyara kuwachiliwa huru.

Wakazi wa kaskazini mashariki mwa Nigeria wanasema kuwa washukiwa na kundi la Boko haramu wamelilipua daraja moja karibu na eneo ambalo wasichana 200 walitekwanyara yapata mwezi mmoja uliopita.
Daraja hilo lililopo katika barabara muhimu ni la pili kuharibiwa katika kipindi cha siku mbili.
Inasemekana kuwa ulipuaji wa daraja hilo ni mpango wa wanamgambo hao kuwazuia wale wanaotaka kuwanusuru wasichana hao kutofika eneo hilo. Mke wa rais wa Marekani Michelle Obama ameelezea utekajinyara wa wasichana hao kama kitendo cha kihuni kinacholenga kudidimiza ndoto za wasichana hao.
Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger