JE! ALICHOKIAZIMIA NKURUNZINZA KINAKIUKA KATIBA?


Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, amegusia kuwa huenda akawania urais kwa muhula wa tatu licha ya upinzani  kulalamika kuwa hatua kama hiyo itakuwa inakiuka katiba.
Bwana Nkurunziza alizungumza kuwa maelezo katika katiba kuhusu jambo hilo hayaeleweki kwa misingi hiyo na kwamba yanahitaji ufafanuzi. Alisema kuwa ikiwa chama chake kitamuomba kuwania urais kwa muhula wa tatu, litakuwa swala linalohitaji kufafanuliwa na mahakama ya kikatiba.
Hali ya wasiwasi ya kisiasa nchini Burundi katika miezi ya hivi karibuni kuhusu hatua ya serikali kujaribu kubadilisha katiba. Wanachama wa upinzani, baadhi ambao wamekamatwa, wanasema hatua hiyo itawakera wengi hasa kwa msingi ya kikabila.

Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger