Mwili wa askari baada ya kupigwa mapanga ya kichwa na majambazi hayo kabla ya kupelekwa hospitali
Na Azminah Khan:
Mnamo 11/06/14 majira ya 0100hrs huko kituo kidogo cha Kimanzichana Pwani, watu wasiojulikana waliojifanya kuwa ni raia wema
waliingia kituo kidogo cha Polisi Kiman nanzi Chana huku wakikimbia wakiwa na silaha za jadi kiasi cha askari wa zamu kuamini kuwa
ni watu wanaohitaji msaada. Cha kushangaza
watu hao walimvamia askari mwenye silaha
ambaye amefahamika kwa jina la JOSEPH
NGONYANI na kuanza kumkatakata mapanga
na hatimaye kupora silaha SMG ikiwa na risasi
30. Ndipo walipoanza kushambulia kwa risasi
askari wengine na kufanikiwa kupora SMG ya
pili na risasi 30. Hatimaye watu hao wakapora
risasi za akiba 41 na kutoweka kusikojulikana.
Askari Ngonyani alifariki dunia alipokuwa
anapatiwa matibabu kwenye hospitali wilaya ya
Mkuranga. Askari mwingine aitwaye VENANCE
amejeruhiwa mgongoni kwa risasi ambayo bado
imo ndani, na kwenye paja la mguu wa kulia.
Mgambo Mariam alijeruhiwa kichwani, shingoni
na kuvimba bega kutokana na kupigwa sana
mateke na kujeruhiwa mbavuni. Kwa mujibu wa mganga Mkuu wa zamu wa Hospitali hiyo aitwaye VERONICA MUSIME, anathibitisha askari huyo kufariki akiwa anapatiwa matibabu hapo Mkuranga wakati wengine wamekimbizwa Muhimbili kwa matibabu ya kina. Kazi ya Mungu haina makosa; vituoni tuwe makini sana na stahili hii ya ujambazi; HESHIMA PEKEE kwa marehemu na majeruhi hawa ni kuwapata watuhumiwa wote na silaha walizoiba bila kuchelewa. Bila kujali mkoa ulipo, taarifa za haraka tunatarajia kupata toka kwako kuhusiana na wahusika wa tukio hili. AMEN
mateke na kujeruhiwa mbavuni. Kwa mujibu wa mganga Mkuu wa zamu wa Hospitali hiyo aitwaye VERONICA MUSIME, anathibitisha askari huyo kufariki akiwa anapatiwa matibabu hapo Mkuranga wakati wengine wamekimbizwa Muhimbili kwa matibabu ya kina. Kazi ya Mungu haina makosa; vituoni tuwe makini sana na stahili hii ya ujambazi; HESHIMA PEKEE kwa marehemu na majeruhi hawa ni kuwapata watuhumiwa wote na silaha walizoiba bila kuchelewa. Bila kujali mkoa ulipo, taarifa za haraka tunatarajia kupata toka kwako kuhusiana na wahusika wa tukio hili. AMEN
Mwili wa Askari mara tu baada ya kujeruhiwa na mapanga na majambazi hayo
mwili huo kesho utasafirishwa na kupelekwa kijiji cha nyumbani kwa marehemu huko Songea
THE BANTU inawapa pole wafiwa wa marehemu askari huyu.



Chapisha Maoni