MAELFU YA WATU WAHUDHURIA MAZISHI YA MAREHEMU MZEE MUSHI HAPO JANA MWEMBEYANGA

Hawa ni baadhi ya watu waliohudhuria Mazishi ya marehemu Mzee Mushi hapo jana katika viwanja vya Mwembe Yanga

Marehemu Mzee Mushi ni moja ya viongozi wa kubwa wa harakati za kiislamu hapa nchini.Kwa muda wa miaka isiyopungua hamsini amekuwa akishughulikia mambo ya harakati za kiislamu, lakini pia yeye alikuwa ni Mwenyekiti wa taasisi ya Almalid Islamic Propagation Center lakini pia akiwa kama ni kiongozi wa wadhamini wa taasisi hiyo wakishirikiana na Mhadhiri Sheikh Riko na wengineo.

Mzee Mushi alifanya mengi sana ambayo anastahiki kuigwa, kwani katika moja ya mambo aliyoyafanya ni kulea watoto yatima katika majumba yake mwenyewe binafsi, lakini pia kuwasomesha watoto hao kuanzia darasa la kwanza hadi vyuo vikuu na ametoa viwanja vingi kwa ajili ya ujenzi wa Madrasa na Misikiti pamoja na ofisi za kuendeshea maswala ya dini hapa nchini.

Mzee Mushi alifariki kutokana na maradhi yaliyokuwa ya kimsumbua kwa muda mrefu, na alifia Dubai akiwa safarini kuelekea India kwa ajili ya matibabu zaidi.

sikui chache kabla ya kifo chake marehemu Mzee Mushi alizungumza maneno haya "endapo nitakuwa nimefanya matibabu na kupona nikarudi katika aafya yangu ya kawaida, basi nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu kuhakikisha tunaandaa mikakati mipya ya kuongeza nguvu katika ufikishaji wa daawa kwa waislamu lakini pia endapo Allah atanichukua basi waislamu jitahidini kuandaa mikakati ya kuendeleza daawa"

PICHA MBALIMBALI


Mwandishi wa THE BANTU akisalimiana na bingwa wa uchumi nchini Mheshimiwa Profesa Ibrahim Lipumba mara tu baada ya kumaliza kuswalia marehemu Mzee Mushi


Mwanadada Asia Iddi rafikiwa wa watoto wa marehemu Mzee Mushi akiwa katika majonzi makubwa ya kuondokewa na Mzee wa rafiki zake wapendwa


 Hawa ni baadhi ya watu waliohudhuria mazishi ya marehemu Mzee Mushi jana

Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger