WAATHIRIKA WA SHAMBULIO LA MWAKA 1998 WALIPWA FIDIA TANZANIA
Hili ni shambulizi la kigaidi lililotikisa Tanzania mwaka 1998 Watanzania walioathirika na mlipuko wa mabomu katika ubalozi wa Marekani yaliyopangwa na Osama bin Laden mjini Dar es Salaam wameshinda kesi yao na sasa watalipwa fidia. Katika hukumu iliyotolewa na Jaji wa mahakama kuu ya Marekani Thomas Bates mjini Columbas, familia tisa za watu waliokufa na waliojeruhiwa watalipwa jumla ya dola laki nne na ishirini za Marekani. Hukumu hii inakuja kufuatia kesi iliyofunguliwa mwaka 2000 kwa msaada wa wanasheria wa kimarekani. Jaji aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo, huyo alitoa hukumu ya awali tangu mwaka 2011 na kilichokuwa kimebaki ni utoaji wa fidia hiyo. Mmoja wa waathirika hao Judith Mwila ambaye mume wake alifariki katika mkasa huo, amesema kuwa yeye amepata taarifa hiyo kupitia kwenye gazeti tu. Msim...