Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2013

LANA:MWANAMKE AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MITANO JELA BAADA YA KUMTUPA MTOTO WAKE CHOONI

Picha
Mwanamke mmoja mkazi wa Manga A Jijini Mbeya amehukumiwa kifungo cha miaka  5 jela kwa kosa la kutupa mtoto wake chooni. Tukio hilo lilitokea Juni 14, Mwaka huu katika eneo hilo baada ya watoto waliokuwa wakicheza  kugundua kuwepo kwa Mtoto katika choo cha shimo.   Mtuhumiwa baada ya kukamatwa amekiri kutenda kosa hilo na kwamba alifanya hivyo baada ya mzazi mwenzie kumkataa. Ameongeza kuwa amelazimika kutupa katika choo cha jirani kwa sababu ni cha shimo  tofauti na chao ambacho asingeweza kutupa mtoto huyo.    Rukia Haruna (31)  akitolewa nje  na Askari wa Jeshi la Polisi akitolewa nje  ya  Mahakama kwenda Gerezani kutumikia kifungo cha miaka 5 Jela     Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Archiles Mulisa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, Zabibu Mpangula, amemtaja Mtuhumiwa kuwa ni Rukia Haruna (31) mkazi wa Manga A Jijini Mbeya na kw...

UNAYAJUA MADHARA YA UVAAJI WA SRUALI ZA KUBANA KWA WANAUME-SOMA MAKALA HII

Picha
Madaktari wamesema uvaaji wa suruali za kubana kwa wanaume ni chanzo cha baadhi kuwa wagumba na wengine kupata magonjwa ya ngozi Kampala. Kwa wananchi wa Uganda, jina la Denzel Mwiyeretsi siyo geni kwa kuwa ni mtangazaji wa masuala ya mjini katika Kituo cha Televisheni cha XFM, lakini Denzel pia ni maarufu kwa wafuatiliaji wa Big Brother kutokana na kushiriki shindano hilo nchini Afrika Kusini. Hata hivyo, watu wengi wanamfahamu kwa mitindo ya uvaaji wake wa suruali za kubana. “Mitindo ni kama umri, haiwezi kuwa vilevile. Ni kama vile mvinyo mtamu, pamoja na umri, mtindo wako lazima uwe na mwonekano mzuri. Ni kujaribu kitu kipya. Mimi ni mtu mwenye kuthubutu na napenda kujaribu vitu vipya (ikiwamo mitindo) ili kufanya maisha yangu yawe yenye mvuto,” alisema Denzel. Pamoja na tabia yake ya kupenda kuvaa suruali za kubana kuna watu akiwamo dada yake hakupendezwa na hali...

MCHEZJI WA ZAMANI WA MANCHESTER UNITED QUINTON FORTUNE ATEMBELEA AZAM CHAMAZI COMPLEX - ASHANGAZWA NA UBORA WAKE

Picha
Quinton Fortune, Mchezaji wa zamani wa Manchester United ambaye kwa sasa anasomea fani ya ualimu wa soka kwenye kompaundi ya Manchester United alipotembelea Azam FC Chamazi leo kwa mwaliko wa DHL,  Fortune alishangazwa na ubora wa Center ya Azam FC na kusema hajawahi kuona kitu kama hiki kinachomilikiwa na klabu hata kwenye nchi yake ya Afrika ya Kusini hakuna klabu inayomiliki Academy kama hiyo ya Azam fc ya  Tanzania

HIVI NDIYO SIRI YA MAISHA YA OSAMA BIN LADEN KABLA YA KIFO CHAKE ILIYOFICHULIWA NA TUME YA ABBOTTABAD

Picha
TUME ya Abbottabad imesema kuwa Osama bin Laden aliishi kama mtu wa kawaida bila wasiwasi wowote kwa karibu miaka 10 na aliwahi hata kusimamishwa na polisi katika eneo la Swat huko Pakistan kwa kupeleka gari kwa kasi mno, lakini hakukamatwa. Ripoti hiyo iliyofichuliwa na Televisheni ya al Jazeera na kuoneshwa juzi jioni, inaonesha kinagaubaga maelezo ya kusisimua kuhusu maisha ya Osama bin Laden, mtu hatari aliyekuwa akitafutwa kwa udi na uvumba, na aliyekuwa akivaa kofia la mchunga ng’ombe katika tambarare za Marekani, kuepuka kugunduliwa kutoka angani. Ripoti hiyo ya kurasa 336, iliandikwa na tume ya Abbottabad inayoongozwa na jaji na iliyoundwa na Serikali ya Pakistan muda mfupi baada ya vikosi maalumu vya Marekani kumuua bin Laden Mei 2 mwaka 2011. Misingi ya ripoti hiyo ni mahojiano yaliyofanywa na vyanzo 201, wakiwemo jamaa wa familia yake na maofisa mbalimbali. Matokeo ya uchunguzi huo ambayo hayajachapishwa rasmi, yanajumuisha ushahidi wa uzembe mkub...