Mwendesha mashtaka mkuu nchini Misri
Mwendesha mashtaka nchini Misri amewafungulia
mashtaka watu 200 wanaodaiwa kuwa wanachama wa kundi moja la waislamu
wenye itikadi kali kutokana na misururu ya mashambulizi dhidi ya vitengo
vya usalama.
Hatahivyo hakuna terehe iliotolewa ya kuanza kusikizwa kwa kesi dhidi ya wanachama hao wa kundi la Ansar Bet Al maqdis.
Takriban wanacham 100 wa kundi hilo ambao kesi zao ziko tayari kuanza hawajulikani waliko. Kundi hilo limekiri kutekeleza mashambulizi
kadhaa , mengi yakifanywa baada ya kuondolewa madarakani kwa aliyekuwa
rais wa taifa hilo Mohammed Morsi. Maafisa wamelishtumu kundi la Muslim Brotherhood kwa kupanga ghasia hizo madai ambayo yamepingwa na kundi hilo.
Chapisha Maoni