SUAREZ AWATIMULIA VUMBI REAL MADRID, BARCELONA NA JEURI YAO YA PESA, ASEMA MAJOGOO NDIO HABARI YA MJINI

Mshambuliaji Luis Suarez amesema hana mpango wa kuondoka Liverpool licha ya kutakiwa na vigogo wa La Liga, Real Madrid na Barcelona
MSHAMBULIAJI Luis Suarez amesema anapenda maisha ndani ya Liverpool na hafikirii kuondoka Anfield.Nyota huyo wa Uruguay amemaliza msimu vizuri akiwa na Wekundu hao wa Anfield kwa kufunga mabao 31 na kutwaa tuzo za Mwanasoka Bora wa Chama cha Wachezaji wa Kulipwa (PFA) na ya Waandishi wa Habari za Soka.Mafanikio hayo yanakuja baada ya kupitia msimu mgumu uliopita akifungiwa kwa kumng'ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic - akilazimisha kupita.
Sasa wakati tetesi za usajili zimeanza tena, Suarez, ambaye mapema wiki hii alikanusha kuwa na nia ya kuhamia klabu nyingine kubwa Ulaya, ameamua kuuheshimu mkataba aliosaini Desemba mwaka jana.
Furaha: Suarez alisaini mkataba mpya mapema msimu uliopita na amesema ana furaha kuwepo Liverpool
Tuzo: Nyota huyo wa Uruguay alishinda tuzo ya mwaka ya PFA, huku Eden Hazard akishinda tuzo ya mchezaji bora kijana wa mwaka.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 ambaye ameripotiwa kutakiwa na Real Madrid, ameiambia Sky Sports kwamba: "Nilisaini mkataba kwa sababu napapenda haps na nina furaha dana hapa. Ikiwa haunt furaha hapa huwezi kusaini mkataba wowote,".
"Liverpool kwangu ni moja ya timu bora duniani, kwa sababu hakuna mtu haps katika chumba cha kubadilishia nguo anafikiri mimi no bora zaidi ya wengine na watu hapa ndani ya Melwood wanafanya kazi vizuri,"alisema.
Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger