UN YASHUTUMU KUULIWA KWA MWANADADA WA KIPAKISTANI


Kamishna wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa, Navi Pillay, aliyeshutumu mauaji ya mwanamke wa Pakistan.

Kamishna wa Umoja wa Mataifa anayesimamia Haki za Kibinadamu, Navi Pillay, amejiunga na maelfu ya watu duniani wanaoshutumu vikali mauaji ya mwanamke Mpakistani aliyepigwa mawe hadi kufa nje ya mahakama na wanachama wa familia yake kwa madai ya kuolewa na mwanamume aliyempenda.

Mume wa mwanamke huyo - Mohammed Iqbal - alisema kuwa alishtushwa na kukasirishwa na maafisa wa polisi waliokuwepo karibu na mahali palipotokea kitendo hicho lakini wakakosa kufanya lo lote kunusuru maisha yake.

"Kilichotokea ni kibaya sana. Mmoja wa jamaa yangu alivua shati na kuwapungia maafisa wa polisi ili waweze kuingilia lakini wakapuuza. Walishuhudia kimyakimya tu Farzana akiuawa na wao hawakufanya lo lote," alisema Iqbal.

Mamia ya wanawake huuliwa kila mwaka nchini Pakistan kwa kuolewa na watu wasiopendwa na familia zao, jambo ambalo halikubaliwi katika jamii nyingi ambazo hazipendelei maisha mamboleo yanayotambua watu kupendana kabla ya kuoana.

Makundi mbalimbali ya kupigania haki za kibinadamu kote duniani hutoa wito kwa Serikali ya Pakistan kuhakikisha kuwa wanaoshiriki mauaji kama haya wanashtakiwa; lakini juhudi zao zimeambulia patupu.
Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger