WANAJESHI WAMSHAMBULIA KAMANDA (NIGERIA)




Wanjeshi hao wamemlaumu kamanda wao kwa kusababisha mauaji ya wenzao

Wanajeshi nchini Nigeria, wamemfyatulia risasi kamanda wao mkuu katika mji wa Maiduguri Kaskazini Mashariki mwa nchi.


Hata hivyo Meja Jenerali, Ahmed Mohammed alinusurika kifo. Shambulizi lilifanywa dhidi ya gari lake katika kambi ya jeshi ya Maimalari .




Wanajeshi hao walimlaumu kamanda kwa mauaji ya wanajeshi wenzao walioshambuliwa na kundi la Boko Haram na kuuawa.


Wakati huohuo, Rais wa Goodluck Jonathan amesema hayuko tayari kubadilishana wasichana miambili waliotekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram wanaozuiliwa katika magereza ya Nigeria.


 Wazazi wa wasichana waliotekwa nyara na Boko Haram

Waziri wa serikali awali alikuwa amesema kuwa maafisa wa utawala walikuwa tayari kwa mazungumzo na Boko Haram lakini Rais Goodluck Jonathan amesisitiza kwamba swala hilo halitazungumziwa.


“Amesisitiza kwamba hataongea na Boko Haram kuhusu kubadilishana wasichana waliotekwa na wapiganaji wa kundi hilo wanaozuiliwa nchini humo,” alisema mwakilishi wa serikali ya Uingereza Mark Simmonds baada ya kukutana na Rais Jonathan kujadili namna ya kuwanusuru wasichana hao.

Hatua ya kutekwa nyara kwa wasichana hao katika jimbo la Borno tarehe 14 Aprili, imesababisha kero kubwa kwa jamii ya kimataifa kiasi cha kulazimisha baadhi ya nchi za kutoa wataalamu kusaidia serikali ya Nigeria kuwatafuta wasichana hao
Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger