Wanjeshi hao wamemlaumu kamanda wao kwa kusababisha mauaji ya wenzao 
Wanajeshi nchini Nigeria, wamemfyatulia risasi kamanda wao mkuu katika mji wa Maiduguri Kaskazini Mashariki mwa nchi.
Hata hivyo Meja Jenerali, Ahmed Mohammed 
alinusurika kifo. Shambulizi lilifanywa dhidi ya gari lake katika kambi 
ya jeshi ya Maimalari .
Wanajeshi hao walimlaumu kamanda kwa mauaji ya wanajeshi wenzao walioshambuliwa na kundi la Boko Haram na kuuawa.
Wakati huohuo, Rais wa Goodluck Jonathan amesema
 hayuko tayari kubadilishana wasichana miambili waliotekwa nyara na 
wapiganaji wa Boko Haram wanaozuiliwa katika magereza ya Nigeria.
 Wazazi wa wasichana waliotekwa nyara na Boko Haram
Waziri wa serikali awali alikuwa amesema kuwa 
maafisa wa utawala walikuwa tayari kwa mazungumzo na Boko Haram lakini 
Rais Goodluck Jonathan amesisitiza kwamba swala hilo halitazungumziwa.
“Amesisitiza kwamba hataongea na Boko Haram 
kuhusu kubadilishana wasichana waliotekwa na wapiganaji wa kundi hilo 
wanaozuiliwa nchini humo,” alisema mwakilishi wa serikali ya Uingereza 
Mark Simmonds baada ya kukutana na Rais Jonathan kujadili namna ya 
kuwanusuru wasichana hao.
                     Hatua ya kutekwa nyara kwa wasichana hao katika 
jimbo la Borno tarehe 14 Aprili, imesababisha kero kubwa kwa jamii ya 
kimataifa kiasi cha kulazimisha  baadhi ya nchi za kutoa wataalamu 
kusaidia serikali ya Nigeria kuwatafuta wasichana hao

 
Chapisha Maoni