Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2014

MADHARA YATOKANAYO NA KUANGALIA SANA TV (TELEVISION)

Picha
  Watu wanaotazama runinga kwa saa tatu au zaidi kila siku wako katika hatari ya kuaga dunia mapema kuwaliko wale wanaotazama kwa muda mchache. Hii ni kwa mujibu wa uchunguzi uliochapishwa katika jarida la the American Heart Association nchini Marekani.   "Utazamaji sana wa wa runinga ni tabia ya watu wasio na kazi ya kufanyatu na kuna ongezeko la mienendo ya kila aina ya tabia za kukaa tu," mtafiti mkuu Miguel Martinez-Gonzalez, profesa wa chuo kikuu cha Navarra iliyoko Pamplona, nchini Uhispania, alisema katika taarifa ya shirika hilo. "Matokeo ya utafiti wetu ni sambamba na utafiti tuliowahi kufanya, ambapo muda unaotumiwa kutazama runinga uliolinganishwa na idadi ya vifo vinavyotokea kwa sababu hiyo."   Watafiti hao waliwachunguz vijana wachanga 13,284 kutoka Uhispania wenye afya na waliohitimu chuo kikuu kuhusu aina tatu ya tabia za kukaa tu na hatari ya kuaga dunia kutokana na sababu zote:muda wa kutazama runinga, muda ...

AJALI MBAYA YATOKEA MAFINGA

Picha
baada ya ajali hiyo,  Inavyoonekana kwa nyuma hii ni sehemu ya mbele ya gari hilo Scania lililogongwa kwa nyuma Sehemu ambayo gari hilo dogo liliingia AJALI mbaya iliyohusisha gari dogo aina ya Land Rover Freelander lenye namba T368 CVK na roli la mizigo aina ya Scania lenye namba T346 BRF imetokea usiku wa juzi katika eneo la Lugemba, kilomita kadhaa kabla ya kufika mji wa Mafinga. Taarifa za awali zinaonesha kwamba dereva wa gari hilo jina lake bado halijapatikana alifariki papohapo baada ya gari yake kuingia mvunguni mwa roli hilo lililokuwa limepaki kandokando ya barabara ya Mafinga Mkoani Iringa, akiwa katika mwendo mkali. Mwanafunzi wa kike wa Chuo Kikuu cha Tumaini aliyekuwemo katika gari hilo amenusurika kufa; binti huyo ambaye pia jina lake halikupatikana amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Mufindi baada ya kujeruhiwa vibaya ikiwa ni pamoja na kukatika mkono. Mashu...

ONA AJALI MNBAYA ILIYOTOKEA LEO MAKONGO DAR ES SALAAM

Picha
Watu kadhaa wameripotiwa kufariki Dunia kwenye ajali mbaya iliyohusisha magari matatu ikiwemo lori la mchanga huku mawili yakiwa ni ya abiria maarufu kama daladala  yanayofanya safari zake kati ya ubungo na Tegeta.   Ajali hiyo imetokea mchana kwenye eneo la kikosi cha jeshi cha Lugalo jijini Dar es salaam. Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo mbaya iliyosababisha vifo vya watu 6, watatu wakiwa ni wanaume na watatu wakiwa ni wanawake huku hali za majeruhi ambao walikimbizwa hospitali ya Lugalo zikielezwa kuwa ni mbaya. Bado jeshi la Polisi limeendelea na uchunguzi kujua iwapo dereva wa daladala hiyo lenye nambari za usajili T 377 BEF aliyesababisha ajali hiyo kama alifanya uzembe ama la. ONA PICHA ZAIDI

JUMUIYA YA WNARUFIJI WA MUSLIM UNIVERSITY OF MOROGORO WAKAA KIKAO KIZITO KUJADILI RUFIJI YAO

Picha
Katibu mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya ya Rufiji Pwani akizungumza katika kikao kilichofanyika juzi cha Wanajumuiya ya Watu wa Rufiji Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro hapo  Mambo Club mjini Morogoro Mheshimiwa Musa alizungumza mengi sana kuhusu Rufiji na hasa katika swala zima la sekta ya elimu, imeonekana kuwa swala la elimu Rufiji ni tatizo sana kiasi ambacho kwamba kunasababisha kuwepo kwa maendeleo duni. Mheshimimwa Musa alisisitiza sana swala la kurudi nyumbani (Rufiji) kwa lengo la kufanya kazi kwa wanarufiji ambao wanategemea kumaliza degree zao hivi karibuni baada ya mwezi mmoja. Mheshimiwa Musa alielezea kuhusu urudishwaji wa fedha za mradi wa maji amabao ungeweza kiuwasaidia warufiji kuondokana na tatizo la maji na yote haya ni kutokana kushindwa kuzitumia pesa zile kwa ajili ya mradi huo. lakini pia mheshimiwa alisema kuwa sekta nyingi Rufiji zinaongozwa na watu ambao si wazawa wa rufiji na wakati huo huo warufiji ambao ni wasomi wapo lakini wana...

WATU TAKRIBAN 34 WAUAWA KWA SHAMBULIZI KENYA

Picha
Watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Kiislamu wameshambulia kituo cha polisi na mahoteli na vijiji mjini Mpeketoni, pwani ya Kenya .  Makabiliano makali yameripotiwa sehemu kubwa ya Jumapili usiku huku wakaazi wakitorokea maeneo ya msitu karibu na kisiwa cha Lamu.. Shirika la msalaba mwekundu linasema kuwa hadi kufikia sasa watu 34 wanahofiwa kuuawa kartika shambulizi hilo lililotokea usiku wa kuamkia leo. Hata hivyo vyombo vya habari vinasema idadi hiyo huenda ikawa watu 47. Shambulizi lilifanyika usiku wa kuamkia leo watu waliokuwa wamejifunika nyuso zao wakiwa wamejihami vikali walivamia vituop vya polisi , hoteli na benki. Shambulizi hilo linakuja siku kadhaa baada ya serikali ya Uingereza kufunga ofisi zake kwa hofu ya usalama. Duru za jeshi la Kenya zimearifu kuwa wapiganaji hao hawajajitambulisha ni wa kundi gani. Baadhi ya walioshuhudia wamesema kuwa wameona maiti kadhaa na majeruhi wengi japo Polisi hawajathibitisha ni watu wangapi wameuawa. Kenya imekumbwa na mashambu...

VICHWA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNE 16 2014

Picha

UFARANSA YAANZA VIZURI MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA 2014. YAICHARAZA HONDURAS MABAO 3 - 0

Picha
Karim Benzema akishangilia bao lake la kwanza aliloliingiza kimyani kwa mkwaju wa penati Timu ya taifa ya soka ya ufaransa imeanza vizuri leo katika michuano ya kombe la dunia mwaka 2014. Ufaransa kwa ujumla wa magoli yote matatu yamepatikana kutoka kwa Karim Benzema kutokana na kazi pamoja na juhudi kubwa alizozifanya katika kuyatafuta magoli hayo. BOFYA HAPO JUU UONE MAGOLI YA KARIM BENZEMA DHIDI YA HONDURAS

CHRISTOPHER MTIKILA AIBWAGA TENA SERIKALI

Picha
MAHAKAMA ya Afrika inayoshughulikia masuala ya haki za binadamu, jana imetoa hukumu katika kesi iliyofunguliwa na Mchungaji Christopher Mtikila, ambayo italazimisha kusitishwa kwa Bunge la Katiba ili kupisha utekelezaji wa sehemu ya hukumu hiyo ambayo ni ya kikatiba. Katika hukumu hiyo, mahakama imeitaka serikali kutekeleza kwa vitendo hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu Juni 14, mwaka jana katika kesi ya kudai mgombea binafsi katika uchaguzi wa ngazi zote, iliyofunguliwa na Mchungaji Mtikila dhidi ya serikali. Akisoma hukumu hiyo, Rais wa majaji wa mahakama hiyo, Jaji  Sophia Akuffor, mbele ya wawakilishi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, alitaka serikali ndani ya miezi sita kwanza kutangaza katika gazeti la serikali hukumu iliyompa ushindi Mchungaji Mtikila ya mgombea binafsi na pia kutangaza hukumu hiyo katika wavuti ya serikali. Jaji huyo aliitaka serikali kuwasilisha katika mahakama hiyo utekelezaji wa hukumu hiyo na kubainisha kuwa imeweka katika mchakato suala la ...

MHESHIMIWA MTEMVU ATOA MISAADA YA VIFAA VYA MICHEZO NA FEDHA KWA MIRADI YA MAENDELEO YA JAMII NA VIKUNDI TEMEKE

Picha
Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu (AM)  akimkabidhi jezi kwa Mwenyekiti wa Umoj wa Umoja wa Vijana wa CCM Kata ya Kilakala Hashim Swedi (wapili kulia), alipotoa jozi nane za jezi hizo na mipira minane kwa ajili ya timu za vijana kwenye kata hiyo leo, katika hafa iliyofanyika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam. Mtemvu ametoa vifaa hivyo kutimiza ahadi aliyotoa alipofanya ziara kwenye kata hiyo siku kadhaa zilizopita. Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Kilakala, Hashim Swedi akishukuru baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo na Mtemvu Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu akikabidhi sh. milioni 1.5 kwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Mtoni jimboni humo, Omry Mateso (kulia), katika hafla iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam, leo. Fedha hizo ni kwa ajili ya kuendeleza ujezi wa jengo la Ofisi ya Serikali ya Mtaa huo.  Katika hafla hiyo zaidi ya vikundi 25 vilipatiwa mamilioni ya fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo...

JAMAA AMUUA MWENZIE NA KUMKATAKATA NA KUUTAFUNA MOYO WAKE AFRKA YA KUSINI

Picha
Mtuhumiwa alipatikana akila moyo wa binadamu kwa kisu na uma Polisi nchini Afrika Kusini wanachunguza tukio ambapo mwanamume mmoja anaripotiwa kumuaa mwanamue mwingine aliyekuwa na uhusiano na kimapenzi na mwanamke anayeaminika kuwa ni mpenzi wake wa zamani. Alimuua ka kumkatakata vipande na kisha kuula Moyo wake.  Majirani eneo la Malunga lililo katika mji wa Gugulethu nje ya mji wa Capetown, wanasema kuwa walikumbana na mwanamume aliyeshuhudia mauaji hayo siku ya Jumanne.  Walioshuhudia wanasema kuwa wakati walipofika katika mtaa wa kifaharai ambako mshukiwa alikuwa anaishi walimsikia akisema kuwa "ni yeye mfalme" akisema kuwa bado anampenda mpenzi wake wa zamani. Kwa sasa anazuiliwa na polisi Polisi mmoja aliiambia BBC kuwa wakati walipowasili eneo la tukio walimpata mshukiwa akila moyo wa binadamu akitumia uma na kisu. Walifahamishwa kuwa mwathiriwa alidungwa kisu upande wake wa kushoto kifuani na kwenye shingo lake na katika sehemu ya uso alikuwa na al...

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNE 13 2014

Picha