SERIKALI YATOA BEI ELEKEZI YA SUKARI

 
HATIMAYE  Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli  imekisikia kilio cha muda mrefu  cha Wananchi ambao  walikuwa wakilalamika kupanda  kwa  bei ya sukari nchini.

Akizungumza na Waandishi wa Habari  mchana huu  jijini Dar es Salaam Mkurugenzi  mkuu wa Bodi ya Sukari nchini,Henry Semwaza amesema kuanzia sasa kilo moja ya  sukari itauzwa sh.  1800 nchi nzima.

"Serikali, kupitia bodi ya Sukari Tanzania, inawaarifu wananchi wote kuwa bei ya rejareja ya sukari sasa itakuwa sh. 1,800 kwa kilo moja
. "Amesema Semwaza na kuongeza;

" Wafanyabiashara wote wanapaswa kuzingatia agizo hili, pamoja na kuhakikisha kuwa sukari inaendelea kusambazwa na kuuzwa kwa wananchi bila kuihodhi.

"Maafisa biashara wa mikoa na wilaya watafuatilia na kusimamia utekelezaji wa agizo kuhusu bei elekezi ya sukari, na hawatasita kuchukua hatua stahiki za kisheria kwa wale watakaobainika kupandisha bei ya bidhaa hiyo. "

Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger