BREAKING NEWS: ALIYEKUWA WAZIRI WA ELIMU WA ZAMANI NA MBUNGE WA MUFINDI MH. JOSEPH MUNGAI AFARIKI DUNIA JIONI YA LEO

Image result for Joseph Mungai afariki dunia
Habari zilizotufikia hivi punde kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, zinasema kuwa Aliyewahi kuwa Waziri wa elimu na Utamaduni katika Serikali ya Benjamin W. Mkapa ndugu Joseph Mungai, amefariki dunia majira ya saa 11 jioni.
 
Akithibitisha taarifa hizo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Aminiel Aligaesha, alisema kuwa marehemu Mungai alifikishwa Hospitalini hapo leo baada ya kula kitu kibaya kinachodhaniwa 'Sumu' na kutapika mfululizo hali iliyompelekea kupoteza maisha. 
 
Mwili wa marehemu umehifadhiwa Chumba cha maiti katika Hospitali hiyo ya Taifa ya Muhimbili.

Habari kamili ya msiba huo zitawajia kadri zitakavyokuwa zikitufikia.
Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger