(MUENDELEZO) HUTAZEEKA MAPEMA ENDAPO UTATUMIA MMEA WA MLONGE



Image result for MLONGE
MAAJABU YA MMEA WA MLONGE
Matatizo mengi ya kiafya ni matokeo ya lishe yenye viinilishe duni au hafifu jambo linalopelekea kuwa na kinga ya mwili isiyo na nguvu kupigana na magonjwa mbalimbali. Unaporekebisha usawa huo usio sawa wa kinga yako ya mwili kwa kutumia mimea na lishe zingine mhimu za asili hutakawia kuona matokeo mazuri kwenye afya yako.

Uwezo wa mti wa mlonge kuyaweza yote hayo ni kutokana na kuwa na vitamini, madini mbalimbali na viondowaji sumu vingi kuliko mmea mwingine wowote. Wagonjwa wengi wenye UKIMWI katika sehemu nyingi za afrika magharibi wameripoti kuongezeka kiasi kikubwa cha kinga yao ya mwili baada ya kutumia mlonge kiasi cha kutokuhitaji dawa.

NGUVU, UMAKINI, NGOZI YENYE KUPENDEZA, KUTOZEEKA MAPEMA NA KUPUNGUZA UZITO NA UNENE
Mlonge una viinilishe mhimu vinavyosaidia kuuongezea uwezo mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Vitamini, madini na homoni mhimu zilizomo kwenye mti huu huufanya mwili wako kuwa na usawa unaohitajika kiafya na hivyo kukupa kinga dhidi ya magonjwa mengi bila idadi.

Mlonge una kiinilishe mhimu sana kwa wingi kuliko mmea au mti mwingine wowote duniani mara maelfu kadhaa kiitwacho kwa kitaalamu kama ‘Zeatin’. Zeatin ndiyo hutengeneza seli mpya za ngozi pia huzifanya seli mpya kutengenezwa kwa haraka na kwa wingi zaidi ya zile seli zinazokufa. Hii huleta matokeo mazuri ikiwemo kuondoa mikunjo ya ngozi au ngozi kuzeeka sehemu za uso na sehemu nyingine za mwili na kukupa afya nzuri ya ngozi.

Kwenye mlonge kuna ‘Sulfur’, hii sulfur ni mhimu katika kuunda vitu mhimu kwenye ngozi kama collagen na keratin huku viuaji au viondowaji sumu zaidi ya 30 vinavyopatikana kwenye mlonge ni mhimu kwa ajili ya afya ya ngozi yako.

Mlonge ambao umekuwa ukitumika kwenye vituo vingi vinavyojihusisha na kupunguza uzito huwa una nguvu ya asili ya kupunguza njaa, huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula na kukung’arisha wewe huku ukikuacha na virutubishi vingi mhimu zaidi.

HUIRUDISHA UPYA AFYA YA MWILI WAKO;
Baada ya kufikisha umri wa miaka 30 hivi nguvu zako za mwili huanza kushuka. Mwili wako utaanza kuleta mchonyoto. Utaona unaanza kupoteza umakini nyakati za mchana sababu hukuzingatia nini ule wakati ulipokuwa kijana. Baadhi ya kuharibika kwa afya hakuwezi kurudishwa nyuma ikiwa ni pamoja na kuzorota kwa afya ya meno.

AFYA MBOVU YA MENO INAPELEKEA MAGONJWA KADHAA NA VIFO;
Calcium, Magnesium, Manganese, Potassium, Boron na Vitamini D yote ni madini mhimu ili uwe na meno yenye afya. Magonjwa mengi sugu ni matokeo ya upasuaji wa kwenye kinywa. Kila mtu anapaswa kulinda afya ya meno yake kuanzia leo kwani meno yakishaoza au kuharibika huwa ni vigumu kupona na kurudi kwenye hali yake ya mwanzo. Afya ya meno yako itaamua ni miaka mingapi unaweza kuishi.
Kila mmoja wetu anatakiwa kutimiza wajibu wake linapokuja suala la afya ya mwili wako. Tumia google tafuta taarifa za kile unachokula au kunywa kila siku. Kichwa kitakuuma utakapojua ni nini unakula!. Nenda YouTube angalia video hizi: “Food Matters” na “Dying to have know”. Tafuta kwenye chaneli ya Discovery movie inaitwa “Moringa The Miracle Tree” na video nyingine inaitwa ‘Moringa Oleifera’.

BIDHAA NYINGI ZA AFYA HAZINA AFYA YOYOTE;
Bidhaa nyingi za afya hazina utafiti halisi (genuine) unaojitegemea au zina maelezo kutoka kwa mtengenezaji tu wa hiyo bidhaa. Mlonge una mfululizo wa tafiti za watu wengi na shuhuda za watu kote duniani zaidi ya miaka 4000 iliyopita. Ni mtishamba kwa asilimia 100 unaoota wenyewe.
Matumizi ya mlonge kama kiua vijasumu (antibiotic) kwenye tiba asili yalianza miaka maelefu iliyopita. Mlonge ulitumika kwa mara ya kwanza kama dawa zaidi ya miaka 2000 kabla ya Kristo. Watabibu wazamani wa Misri na Ugiriki waliona faida nyingi za mti huu na wakautambulisha kwa Warumi na baadaye mlonge ukaenea mashariki mwa India na sehemu ya chini ya nchi ya Uchina, kusini mashariki mwa Asia na Ufilipino na magharibi mwa Misri kuzunguka mediterania na mwishowe ukafika kwa Wahindi mashariki mwa Amerika. Leo zaidi ya watu milioni 400 wanatumia mlonge. Shirika la afya duniani (W.H.O) limekuwa likitumia mlonge zaidi ya miaka 40 sasa.
Unga wa majani ya mlonge unapaswa uwe ni wa kijani kweli kweli na majani yake yawe yalianikwa kivulini na siyo juani. Anza na kijiko kidogo kimoja ukichanganya na vimiminika kama maji ya uvuguvugu au juisi yoyote ya matunda uliyotengeneza mwenyewe nyumbani kutwa mara moja na taratibu ongeza kiasi cha dawa kadri unavyohitaji. Unaweza kuuchanganya pia kwenye wali wakati unakula au unaweza kuweka ndani ya kikombe cha uji au unaweza kutumia kama majani yako ya chai ingawa hautakiwi uchemshe sana kwenye moto.

Mti wa mlonge sasa umeanza kuwa maarufu huko Marekani hii ni kutokana na mti wenyewe kuendelea kupata umaarufu miongoni mwa watu wanaojali afya zao. Ingia google andika ‘Moringa plants for sale’ utagundua keyword hiyo inatafutwa kila siku mara maelfu. Watu wengi pia wameanza kilimo cha mlonge kama biashara ya kuwaingizia kipato. Ukiwa na miti 200 tu ya mlonge shambani kwako tayari wewe siyo mwenzetu.

Mti wa mlonge ni moja ya miti mhimu katika sehemu yote ya dunia. Kadri watu wanavyoendelea kuutafiti na kuusoma mti huu ndivyo mahitaji ya unga wa majani yake, mbegu zake, unga wa mbegu zake na mafuta ya mbegu zake yatakavyozidi kuongezeka na kuongezeka

Share this post :

Chapisha Maoni


Get This:Techkgp

PAGE VIEWERS

About Me

Blog Archive

Blog za rafiki zangu

Get This:Techkgp
3D Live Statistics
 
Support : The Bantu | Mufandish | Mufandish Inc
Copyright © 2011. MUFANDISH NEWS - All Rights Reserved
Template Created by Mufandish Inc Published by Mufandish Mufandish
Proudly powered by Blogger