Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Meja Edward Gowele ameagiza kukamatwa kwa Vijana na Wazazi wote wenye watoto ambao wana umri wa kwenda shuleni watakaonekana wanafanya biashara maeneo ya stendi na maeneo mengine muda wa masomo .
Ameyasema hayo katika kikao cha Wadau wa Elimu kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri Wilayani Rufiji.
Sanjari na hilo, amewaonya Wazazi wanaomaliza kesi za mimba kwa watoto wa shule bila kwenda mahakamani na kuwageuza mabinti hao sehemu ya kujipoatia kipato.
Pia ameitaka Jamii kukemea swala la wazazi kuwaacha Watoto wanaosoma kulea familia Jambo linalozorotesha maendeleo yao kielimu.
Gowele ameendelea kuhamasisha Jamii na Wadau mbalimbali wa Elimu kuendelea kuunga Mkono Serikali ya awamu ya sita katika uboreshaji wa miundombinu ya Elimu kwa Shule za Msingi na Sekondari huku akishukuru Bank ya NMB, CAMFED pamoja na mdau kutoka Korea kwa misaada wanayotoa katika kuboresha Elimu Wilayani humo.
Sambamba na hayo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha nyingi za miradi ya Maendeleo hususani katika Elimu kwa Wilaya ya Rufiji na kutoa pongezi kwa Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye mara kwa mara amekuwa akijitoa na kuelekeza nguvu zaidi katika uboreshaji wa huduma za Jamii hususani Elimu kwa kutoa mifuko ya sementi zaidi ya 1000 katika maeneo yenye shule shikizi kwa ajili ya ujenzi wa Madarasa.
Habari Picha
Chapisha Maoni