HARAMBEE STARS KWA KWELI YAAMBULIA PATUPU
Harambee Stars imeondolewa kwenye kinyang'anyiro cha kufuzu kombe la dunia 2014 Mchuano wa kufa na kupona ulishuhudiwa kati ya bingwa wa Afrika Super Eagles wa Nigeria na Harambee Stars wa Kenya katika uwanja wa kimataifa wa Moi Kasarani mjini Nairobi. Musa Ahmed aifungia Nigeria bao la kwanza na la pekee kunako dakika ya 81. Mashabiki wa Kenya Kimya! Baadhi ya mashabiki wa timu ya taifa ya Kenya Harambee Stars waanza kuondoka uwanjani. Mashabiki wa Nigeria hawakuwa wengi uwanjani wakikisiwa kufika 300, lakini licha ya uchache wao ,hawakufa moyo.Mandishi wa BBC Odeo Sirari aliyekuwa uwanjani,alishuhudia mashabiki wachache wa Nigeria wakiisiahngilia timu yao kwa nyimbo na ngoma japo hawakuwa wanasikika kutokana na mayowe ya wakenya. Ilikuwa mechi ya mkondo wa pili kwa timu hizo mbili baada ya kwenda sare ya bao moja kwa moja walipocheza kwa mkondo wa kwanza mjini Calabar Nigeria mwezi jana. Mechi hii ni ya kundi la F ya kugombania nafasi ya kushirik...