Machapisho

CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA WILAYA YA RUFIJI KATIKA KUADHIMISHA SIKUKUU YA MUUNGANO WAMETEMBELEA KITUO CHA AFYA KUWAFARIJI WAGONJWA

Picha
Na: Yussuf Yussuf Chama cha Skauti Wilaya ya Rufiji mapema leo hii wametembelea kituo cha afya cha Ikwiriri kwa lengo la kuwatembelea wagonjwa na kuwafariji ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Chama hicho ni dasturi yao kwa kila matukio ya kitaifa yanapotokea hufanya mambo kama haya ya kujitolea kama ilivyo utamaduni wao. Sambamba na hilo wameweza kupata kujifunza historia hii ya Muungano kutoka kwa wazee walioushuhudia Muungano huo .  

MBUNGE WA JIMBO LA RUFIJI AFUTURISHA MAELFU YA WANANCHI IKWIRIRI RUFIJI

Picha
IKWIRIRI RUFIJI-PWANI  SIKU YA JANA MAWAIDHA YA MBUNGE WA RUFIJI KABLA YA MUDA WA IFTARI. Mbunge wa Rufiji na Waziri wa Mali Asili na Utalii Nchini  Mhe, Mohamed Mchengerwa Kupitia Wana Rufiji Atoa Shukrani za dhati kwa Mhe, Rais Samia Suluhu kuendelee kumtakia kheri kuwa na Afya Njema na Upendo wa dhati kwa Wana Rufiji na Watanzania wote  katika  Kutekeleza Majukumu yake na Maendeleo anayoendelea kuwaletea Wana Rufiji Ameyasema hayo mbele ya wananchi wa Tarafa ya ikwiriri. Ikiwa ni siku ya Pili ya Kufuturisha Wananchi na Wakazi wa Rufiji, Siku ya  Jana Wamejitokeza  wananchi takriban 8500 kwenye Futari ya Ikwiriri ikitanguliwa na Futari ya Utete ya Tarehe 8/4. Aidha Mhe Mchengerwa amewasisitiza wana Rufiji pamoja na Mfungo Mtukufu wa Ramadhani kuzingatia Ibada muhimu ya kufanya Kazi kwani kwa mujibu wa mafundisho ya Dini ya Kiislamu , Kazi ni Ibada iliyotiliwa mkazo na Allah sw na mtume wake Mohammed  saw, hivyo shime kwa wana Rufiji kufanya kazi kwa ...

MRADI WA SHULE BORA NCHINI WAZINDULIWA MKOANI PWANI

Picha
  WAZIRI wa Uingereza anayeshughulikia Afrika, Vicky Ford amesema ndoto yake Ni kuona ufadhili kutoka nchini humo unaleta matokeo chanya nchini Tanzania, kwa kuhakikisha Watoto wenye mahitaji maalum ,wenye Mazingira magumu na watoto wa kike wanapata elimu bora. Aidha amesema ufadhili huo kupitia Shirika la msaada la nchi hiyo, linalenga kufikia watoto milioni nne nchini. Akizindua mradi wa shule bora ,mkoa wa Pwani ukiwa Ni mwenyeji, Ford alisema jamii, Serikali, wadau wa elimu wanapaswa kushirikiana kurudisha wimbi la wanafunzi walioacha shule kwa changamoto mbalimbali waweze kuendelea na masomo. "Tutaweka kipaombele kwa watoto wenye mahitaji maalum,wanaoishi kwenye Mazingira magumu na watoto wa kike, kupata haki ya kuendelea kusoma katika Mazingira bora "alifafanua Ford. Awali Waziri wa elimu, prof.Adolf Mkenda Alieleza mradi huo umefadhiliwa na Uingereza kwa paundi milioni Tisa ,ambapo unafikia mikoa Tisa, ili kuhakikisha Watoto wote hata wenye changamoto mbalimbali wanapa...

TAZAMA FAIDA ZA MBAAZI LEO HII ILI UJUE NAMNA GANI UNAWEZA KUJITIBU KWA KUTUMIA MBAAZI

Picha
Mbaazi ni moja ya dawa za mitishamba zinazotibu mambo mengi ikiwemo kurudisha bikra ya msichana endapo majani yake yatatumika na kuandaliwa vyema. Tuwe makini katika kufuata njia za kuandaa dawa yetu. MAANDALIZI YA KUANDAA MAJANI YA MBAAZI (kwa wanawake) Chukua majani ya mbaazi kisha yatwang Weka maji kidogo vaa kama pedi kwa muda wa wiki utaona mabadiliko FAIDA ZA KUTUMIA MAJANI YA MBAAZI (kwa wanawake) Kukausha uke Kuondoa majimaji ukeni Kuongeza joto ukeni wakati wa jimai Kuongeza hamu ya tendo la ndoa Husogeza kizazi karibu Kusafisha kuta za uke NB : Mbaazi ni mti wenye maajabu makubwa kuanzia Mizizi yake mpaka majani TIBA KWA WATU WOTE Dawa hii inaweza kutibu magonjwa yafuatayo 1-Inauwezo mkubwa wa kushusha homa 2-Husaidia kuponesha vidonda. 3-Husaidia kurekebisha mzunguko wa hedhi kwa wanawake. 4-Husaidia kupunguza uvimbe 5-Huponyesha kifua na kukohoa. 6-Husafisha kibofu/njia ya mkojo. 7- Huongeza kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbali mbali

WALIMU WA SHULE YA SEKONDARI UMWE WAFANYA TAFRIJA YA KUJENGA MAHUSIANO MAZURI LEO KAZINI

Picha
  Walimu wa shule ya Sekondari Umwe iliyopo Kata ya Umwe Tarafa ya Ikwiriri Wilayani Rufiji wafanya tafrija fupi ambayo inalenga kukuza mahusiano mazuri kazini. Tafrija fupi ambayo imeongozwa na Mkuu wa Shule hiyo Ndugu Bakari Elisafi Mfingi ilifanyika kwa kuchinja Mbuzi, Kuku pamoja na chakula cha pamoja. The Bantu ilifanya mahojiano na Mkuu wa Shule hiyo akisema kuwa hii ni sehemu ya utaratibu wetu kama Stuff kujumuika pamoja kwa siku moja kwa kila term tukiwa na dhamira ya kukuza uhusiano kazini kwani tunaamini kuwa mahusiano mazuri kazini ndiyo yanayoleta ufanisi katika utendaji kazi wetu. Alisema Mfingi. Habari Picha

TASSAF KUWAJENGEA WALENGWA NGURYATI KIWANDA KIDOGO

 

"VIONGOZI MSIWATUKANE NA KUWADHALILISHA WATUMISHI WA UMMA MBELE ZA WATU" MH. MCHENGERWA